ADVERTS

LOGO

Search This Blog

Wednesday, June 20, 2012

MUBARAKA HOI

Taarifa za kutatanisha zimeibuka kuhusu afya ya Hosni Mubarak aliyeondolewa madarakani kufuatia maandamano ya kutaka mageuzi nchini Misri mwaka jana.
Baadhi ya vyombo vya habari vimetangaza kuwa uhai wake unasitiriwa kwa kutumia mashine baada ya kuhamishwa kutoka gerezani hadi kwenye hospitali ya kijeshi mjini Cairo.
Hosni Mubarak
Mwezi uliopita alihukumiwa kifungo cha maisha jela
Mubarak mwenye umri wa miaka 84 aliugua kiharusi akiwa jela, hali iliosababisha ahamishwe hadi hospitalini akiwa mahututi.
Kiongozi huyo aliondolewa mamlakani mwaka jana kufuatia maandamano ya raia wa nchi hiyo yakupinga utawala wake.
Mwezi uliopita alihukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kosa la kuamrisha mauaji ya baadhi ya waandamanaji hao.
Mara kadhaa kumekuwepo na taarifa za kutatanisha kuhusu afya ya rais huyo wa zamani lakini kila mara zimepuuzwa.
Taarifa hizo kuhusu afya yake zimetokea wakati ambapo maelfu ya waandamanaji wamekusanyika kwenye bustani ya Tahrir kulaani uamuzi wa baraza la kijeshi wa kujilimbikizia mamlaka.